Tanzania emblem
The United Republic of Tanzania
The Prime Minister's Office

Tanzania Commission for AIDS

Tanzania Commission for AIDS

News

MKUTANO WA USAMBAZAJI WA TAARIFA YA MAPITIO YA FEDHA ZA UKIMWI


Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS)

Dkt.Leonard Maboko amesema jitihada za ziada zinahitajika katika

kuimarisha vyanzo vya ndani vya fedha za kupambana UKIMWI nchini.

Akizungumza wakati wa kufunga kikao cha waratibu wa UKIMWI kutoka

Wizara, Mikoa na Halmashauri kilichofanyika Mkoani Singida cha usambazaji

wa taarifa ya mapitio ya fedha za UKIMWI kwenye sekta za umma na sekta binafsi ya

mwaka 2022

Dkt. Maboko alisema fedha za UKIMWI zinazidi kupungua kwa asilimia 15

mwaka hadi mwaka, hivyo kuwa jitihada za ziada zinahitajika katika

kuimarisha vyanzo vya ndani.

Hadi sasa fedha nyingi zinategemewa katika Mwitikio wa UKIMWI ni zile

zinazotoka kwa wadau wa maendeleo bado hatujafikia pazuri katika vyanzo

vyetu vya ndani (domestic financing) na hata fedha inayopangwa katika

lengo A katika bajeti ya Mwaka katika Wizara na taasisi za Umma

haipatikani ili kutekeleza Malengo yaliyokusudiwa.

Changamoto ni kuwa kama nchi bado hatujaweza kujitegemea wenyewe

katika Mwitikio wa VVU na UKIMWI, licha ya malengo yaliyopo ya kufikia

2030 kuwa kama nchi tuwe tumefikia sifuri tatu, maambukizi mapya sifuri,

vifo viwe vimefikia sifuri na unyanyapaa uwe umefikia sifuri.

Dkt. Maboko alisisitiza kuwa ni kweli kuwa fedha kutoka kwa wafadhili

zinapungua katika miaka miaka 2 hadi mitatu ya nyuma na mwelekeo wa

wa miaka ijayo kupitia vikoa vya watalaamu na wadau wa maendeleo

fedha za mwitikio wa VVU na UKIMWI zinaendelelea kupungua kwa silimia

15.

Aidha wakati wa kongamano la kimataifa la UKIMWI lililofanyika nchini

Canada Mkurugenzi wa UNAIDS Duniani alisema katika miaka3- 5 ijayo

mabilioni ya fedha za UKIMWI zitapungua na hili sio suala la Tanzania

pekee ni changamoto ya nchi zote.

“sasa lazima tuimarishe vyanzo vya fedha za ndani,kwani malengo yapo

pale pale na hatujayafikia na maambukizi mapya kwa mwaka watu 54,000

wanapata maambukizi ya VVU, hii ukichukulia kwa siku watu 147 wanapata

maambukizi mapya, ambapo mwaka 2007 watu 200 walikuwa wanapata

maambukizi mapya.

Takwimu zinaonesha kwamba asilimia 30 ni kwa vijana wa miaka 15 hadi

24, ambapo kwa siku vijana 44 wanapata maambukizi ya VVU, wakati huo

takwimu zinaonesha vijana wa kike 31 wanapata maambukizi ya VVU kwa

siku kupitia takwimu hizi ni wazi kuwa kuna haja ya kuweka nguvu na

raslimali nyingi kwa vijana.

Miradi ya vijana kwa kutegemea wafadhili yaani PEPFAR tupo katika

halamshauri 11 lakini kwenye mipango ya mwaka huu zitafika halmashuri

14 kupitia mradi wa Dreams, wakati Global fund ni halmashauri 18

zilizofikiwa kwahiyo hadi sasa ni halmashauri 32 kati ya halmashauri 187.

Pamoja na upungufu uliopo bado hatujafikia halmashauri zote nchini

kwahiyo ni muhimu, tunapopanga mipango yetu vipaumbele viwe kwa

maeneo ambayo hayajafiwa na wafadhili.