The Tanzania Commission for AIDS
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Ofisi ya Waziri Mkuu

TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA
The Tanzania Commission for AIDS
TACAIDS
English | Kiswahili 
Home Kuhusu TACAIDS
Kuhusu TACAIDS
Usuli Print

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iko Afrika Mashariki. Inashirikiana mipaka na Kenya na Uganda kwa upande wa kaskazini, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa upande wa magharibi, na Malawi, Zambia na Msumbiji kwa upande wa kusini. Bahari ya Hindi inafanya mpaka wa mashariki. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeundwa na Tanzania Bara na Zanzibar. Waraka huu unahusu Tanzania Bara tu. Tanzania Bara imegawanyika kiutawala katika mikoa 21 na wilaya 133, manispaa na halmashauri za miji. Tanzania inakadiriwa kuwa na watu takribani milioni 37 (hesabu ya 2005) ambapo asilimia 30 wanaishi mijini na asilimia 70 wanaishi vijijini. Idadi kubwa ya watu ipo kanda ya Ziwa, katika Ziwa Victoria kwa upande wa kaskazini na kuzunguka Dar es Salaam, kituo kikuu cha biashara katika mwambao, na kusini nyanda za juu katika Mkoa wa Mbeya. Maeneo makubwa ya nchi yana watu wachache waliotawanyika. Kiwango cha ongezeko la watu kinakadiriwa kuwa asilimia 2.8, na umri wa watu kuishi ni miaka 47 kwa wanaume na 49 kwa wanawake, zikiwemo athari za VVU na UKIMWI.

Tanzania ni miongoni mwa nchi maskini duniani yenye Pato Ghafi la Taifa kwa kila mtu kwa mwaka la Dola za Marekani 660. Tanzania ni ya 162 kati ya nchi 177 katika Faharasa ya Maendeleo ya Watu ya UNDP (2004). Umaskini umeenea nchi nzima. Tanzania imeanzisha mpango kabambe wa kupunguza umaskini unaojulikana kama MKUKUTA. Una shabaha ya kupunguza umaskini kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2010. Kwa mujibu wa makadirio ya mwaka 2000/2001 asilimia 36 ya watu wanaendelea kuishi chini ya Kiwango cha Umaskini wa Mahitaji ya Misingi, imepungua asilimia tatu tu ikilinganishwa na miaka 10 iliyotangulia. Kutokana na ongezeko la watu, idadi kubwa ya watu maskini imeongezeka katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Ingawa kiwango cha jumla cha kukua kiuchumi ni kati ya asilimia 5.7 na asilimia 6.7 kuanzia mwaka 2001 hadi 2004, kiwango cha kukua katika sekta ya kilimo kimekuwa cha chini kuliko sehemu nyingine za uchumi. Wakati umaskini unaweza kupungua sana Dar es Salaam, maeneo ya vijijini bila ya shaka huenda yakakosa kufikia shabaha iliyowekwa na MKUKUTA. Hakuna mlingano wa maendeleo nchi nzima na hii ni kwa mujibu wa viashirio mbalimbali. Wilaya chache zina chini ya asilimia 15 ya kaya chini ya kiwango cha umaskini wa mahitaji ya msingi, hali ya kuwa katika wilaya nyingine asilimia inaweza kufikia 60. Hata hivyo baadhi ya wilaya maskini kabisa zimefanikiwa katika kupunguza kiwango cha vifo vya watoto wa chini ya umri wa miaka mitano au kiwango halisi cha uandikishaji elimu ya msingi.

Kwa kawaida maendeleo ya uchumi hayakufikia hadi katika maeneo ya vijijini. Hata hivyo kuna miradi mingi kabambe ya sekta za miundombinu, mawasiliano ya simu, madini na utalii nchini na katika eneo lote la Afrika Mashariki, inayoweza kutoa fursa mpya kwa ajira na mapato katika sekta rasmi na isiyo rasmi. Hata hivyo inaweza kuingiza changamoto mpya kwa sababu kusafiri kutaweza kuongezeka na nyendo za wanaume peke yao nje ya familia zao na jamii kwa kufuata ajira (ya muda). Fursa hizo zinaweza kuweka mazingira ya kuenea kwa haraka kwa VVU na UKIMWI.

 
Kazi za TACAIDS Print

Zifuatazo ni kazi za TACAIDS: -

  1. Kutunga miongozo kwa ajili ya mwitikio wa mapambano dhidi ya janga la UKMIWI na usimamizi wa athari zake Tanzania Bara
  2. Kutayarisha mkakati kwa ajili ya mipango na shughuli za udhibiti wa VVU/UKIMWI kwa mujibu wa mkakati wa Taifa.
  3. Kukuza uhusiano wa kitaifa na kimataifa miongoni mwa wadau wote kupitia uratibu bora wa mipango na shughuli zote za kudhibiti UKIMWI kwa mujibu wa mkakati wa Taifa.
  4. Kutafuta, kugawa kulingana na mahitaji na kufuatilia matumizi yake.
  5. Kusambaza na kubadilishana taarifa kuhusu janga la VVU/UKIMWI na madhara yake nchini Tanzania ili tuweze kudhibiti janga hilo.
  6. Kuhimiza na kuimarisha utafiti, ubadilishanaji taarifa na nyaraka na utunzaji kumbukumbu kwa ajili ya kuzuia na kudhibiti VVU/UKIMWI.
  7. Kuimarisha program za uraghbishi na elimu kwa kiwango cha juu.
  8. Kufuatilia na kutathmini shughuli zote za VVU/UKIMWI
  9. Kuratibu shughuli zote za kudhibiti janga la UKIMWI nchini Tanzania kwa mujibu wa mkakati wa Taifa.
  10. Kuwezesha juhudi za kupatikana tiba na chanjo na kuimarisha upatikanaji wa huduma na matunzo.
  11. Kuilinda haki za jamii ya watu walioathiriwa na walioathirika na VVU/UKIMWI
  12. Kujenga mazingira wezeshi kwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI waweze kukubali hali
  13. Kuishauri serikali kuhusu masuala yote ya udhibiti wa VVU/UKIMWI Tanzania bara.
  14. Kubainisha vikwazo vya utekelezaji wa afua za VVU/UKIMWI katika sera za kinga, mipango na kuhakikisha ufikiwaji wa malengo yaliyowekwa.
  15. Kuimarisha shughuli zote zinazohusu huduma za kinga na udhibiti wa janga la UKIMWI katika yafuatayo:
  • Huduma za afya na ushauri kwa watu wanao ugua UKIMWI
  • Ustawi wa wafiwa, yatima na wategemezi waliobaki.
  • Kushughulikia masuala ya kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na kisheria yanayohusu janga la UKIMWI
  1. Kutekeleza shughuli na majukumu mengine yeyote yanayohusu kinga na udhibiti wa UKIMWI katika Tanzania bara kama Tume itakavyoona inafaa.

 

 
<< Start < Prev 1 2 Next > End >>

Page 2 of 2