The Tanzania Commission for AIDS
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Ofisi ya Waziri Mkuu

TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA
The Tanzania Commission for AIDS
TACAIDS
| English | 
Home Kuhusu TACAIDS Majukumu
Kazi za TACAIDS Print

Zifuatazo ni kazi za TACAIDS: -

  1. Kutunga miongozo kwa ajili ya mwitikio wa mapambano dhidi ya janga la UKMIWI na usimamizi wa athari zake Tanzania Bara
  2. Kutayarisha mkakati kwa ajili ya mipango na shughuli za udhibiti wa VVU/UKIMWI kwa mujibu wa mkakati wa Taifa.
  3. Kukuza uhusiano wa kitaifa na kimataifa miongoni mwa wadau wote kupitia uratibu bora wa mipango na shughuli zote za kudhibiti UKIMWI kwa mujibu wa mkakati wa Taifa.
  4. Kutafuta, kugawa kulingana na mahitaji na kufuatilia matumizi yake.
  5. Kusambaza na kubadilishana taarifa kuhusu janga la VVU/UKIMWI na madhara yake nchini Tanzania ili tuweze kudhibiti janga hilo.
  6. Kuhimiza na kuimarisha utafiti, ubadilishanaji taarifa na nyaraka na utunzaji kumbukumbu kwa ajili ya kuzuia na kudhibiti VVU/UKIMWI.
  7. Kuimarisha program za uraghbishi na elimu kwa kiwango cha juu.
  8. Kufuatilia na kutathmini shughuli zote za VVU/UKIMWI
  9. Kuratibu shughuli zote za kudhibiti janga la UKIMWI nchini Tanzania kwa mujibu wa mkakati wa Taifa.
  10. Kuwezesha juhudi za kupatikana tiba na chanjo na kuimarisha upatikanaji wa huduma na matunzo.
  11. Kuilinda haki za jamii ya watu walioathiriwa na walioathirika na VVU/UKIMWI
  12. Kujenga mazingira wezeshi kwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI waweze kukubali hali
  13. Kuishauri serikali kuhusu masuala yote ya udhibiti wa VVU/UKIMWI Tanzania bara.
  14. Kubainisha vikwazo vya utekelezaji wa afua za VVU/UKIMWI katika sera za kinga, mipango na kuhakikisha ufikiwaji wa malengo yaliyowekwa.
  15. Kuimarisha shughuli zote zinazohusu huduma za kinga na udhibiti wa janga la UKIMWI katika yafuatayo:
  • Huduma za afya na ushauri kwa watu wanao ugua UKIMWI
  • Ustawi wa wafiwa, yatima na wategemezi waliobaki.
  • Kushughulikia masuala ya kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na kisheria yanayohusu janga la UKIMWI
  1. Kutekeleza shughuli na majukumu mengine yeyote yanayohusu kinga na udhibiti wa UKIMWI katika Tanzania bara kama Tume itakavyoona inafaa.