|
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Waziri Mkuu TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA |
|
![]() |
| English | |
| Kinga na Elimu |
|
|
Matibabu ya maambukizo kwa ngono yaliongezeka katika hospitali na vituo vya afya vyote na asilimia 60 ya zahanati; Kumekuwa na ongezeko kubwa la upatikanaji wa kondomu za wanaume nchini (kutoka milioni 50 hadi milioni 150); Vituo vya Unasihi na Upimaji wa Hiari vimeongezeka zaidi ya mara tatu; Uzuiaji wa Uambukizo wa VVU kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto umeongezeka hadi kwenye asilimia 12 ya hospitali na vituo vya afya; Kutokana na utafiti mbalimbali, kulikuwa na uthibitisho kwamba vijana wameanza kubadili mienendo yao ya ngono (ongezeko la kuchelewesha shughuli za ngono, wapenzi wachache wa ngono n.k.) na programu za uendelezaji wa afya shuleni zilipanuliwa, na; Sekta binafsi na zisizo rasmi zimejihusisha zaidi na mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kutoa programu za kinga na matunzo kwa waajiriwa na jamii kwa ujumla.
Soma zaidi
|