|
Ngazi ya mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa |
|
|
Sekretarieti za Mikoa (RSs) zimepewa jukumu la uratibu, usimamizi na kurahisisha kazi kwenye wilaya na jamii.
Kuundwa kwa Wakala za Uwezeshaji za Mikoa. (RFAs), kila moja ikiwakilisha mikoa miwili ilikuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha msaada wa kiufundi na kifedha unaotolewa wilayani na kwenye jamii. RFAs zinaonekana kama macho, masikio na mikono ya TACAIDS. Ziliweza kuchochea kwa kiasi kikubwa, mwitikio wa wilayani kupitia kujenga uwezo na kuelekeza fedha kwenye CSOs. Pia zimekuwa zikitoa msaada wa kiufundi kwa RSs na CMACs. Hata hivyo RFAs zimekuwa changamoto kubwa katika kufikia na kutoa huduma katika mikoa miwili inayoshughulika nayo. Hili lilikuwa tatizo lililosababisha changamoto kwa upande wa ununuzi na usafirishaji, kudhibiti muda na utoshelevu wa rasilimali. Zaidi ya hayo, kutokana na kwamba RFAs hazikuwa kwenye muundo wa serikali, ilisababisha wakati mwingine kutiliwa shaka na wadau katika ngazi ya mikoa na hivyo kuonekana kama chombo mbadala au pinzani.
|
|
Read more...
|
|
Ngazi ya Taifa |
|
|
Kulingana na Kanuni ya Dhana Tatu, Tanzania imeendeleza na kuimarisha miundo ya asasi zake katika kuratibu Mwitikio wa Taifa. Katika ngazi ya taifa, kuanzishwa kwa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Wizara ya Kukabili Majanga na UKIMWI zilikuwa ni hatua dhahiri.Pia kuundwa kwa Kamati ya Ufundi ya Wizara mbalimbali kuhusu UKIMWI (IMTC) kumeongeza msukumo kwenye mwitikio wa UKIMWI nchini. TACAIDS imekuwa ni kiungo muhimu cha kitaifa. Tume hii imekuwa na kazi nyingi zinazoongezeka kila mara kama vile kutoa mwongozo na msaada wa kiufundi kwenye jamii na sekta binafsi nchini.
|
|
Read more...
|
|
|
Ufuatiliaji na Tathmini |
|
|
Lengo: Kutunza vielelezo sahihi na jumuisho vilivyotolewa kwa wakati ili kuwezesha kupanga na kufanya maamuzi kuhusu UKIMWI.
Kiashirio: Asilimia ya watekelezaji wa afua za UKIMWI na VVU wanaotoa taarifa za kushiriki katika semina za UKIMWI katika miezi 12 iliyopita.
Masuala ya kimkakati. Ufuatiliaji na Tathmini ni shughuli muhimu katika mipango ya kimkakati. Zinatoa msingi wa kupima matokeo dhidi ya hatua za utekelezaji zilizokusudiwa. Masuala matano ya kimkakati yameathiri kiwango cha kuwepo kwa takwimu kwa ajili ya kupima utendaji uliopita wa mwitikio wa UKIMWI Tanzania:
- Kutokuwepo kwa mazingira wezeshi kwa ajili ya Ufuatiliaji na Tathmini,
- Kutokuwepo uwianishi wa kutosha wa takwimu na mifumo yake,
- Kutokuwepo mtiririko na ukosefu wa kuhakikisha ubora wa takwimu zilizopokewa,
- Matumizi finyu ya takwimu kwa ajili ya kutolea maamuzi
- Kukosekana kwa ajenda zilizoratibiwa.
|
|
Upunguzaji Athari |
|
|
Watoto walio katika mazingira magumu:
Msaada wa jamii, kwa watoto walio katika mazingira magumu kupitia mwitikio shirikishi unaimarishwa na kusaidiwa na utoaji huduma zilizopanuliwa.
Walioathiriwa:
Uwezo wa watu binafsi, familia na jamii kushughulikia athari za VVU na UKIMWI unaimarishwa. Watu wanaoishi na VVU na UKIMWI
Watu wanaoishi na VVU na UKIMWI (WAVIU) na wadau wengine wanawezeshwa kushughulikia ipasavyo mahitaji na haki kwa WAVIU kwa kuzingatia hali tofauti pamoja na mahitaji ya wanawake na wanaume.
|
|
|
|
|
<< Start < Prev 1 2 Next > End >>
|
|
Page 1 of 2 |