The Tanzania Commission for AIDS
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Ofisi ya Waziri Mkuu

TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA
The Tanzania Commission for AIDS
TACAIDS
English | Kiswahili 
Home Ushirikiano
Wadau
Mfuko wa Maendeleo Print

Kufuatia kukamilika kwa mikataba ya Wakala wa Tume wa Mikoa [RFA], TACAIDS imeingia mkataba na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii ili kuendelea kupeleka fedha za MJADU [CARF] kwa Jamii. Aidha mkataba huu ulilenga kukamilisha utoaji wa fedha kutoka mradi wa TMAP amabo unamalizika mwezi Machi 2010

 
Washirika wa Maendeleo Print

Wafuatao ni baadhi ya Washirika wa Maendeleo wanaoshirikiana na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI nchini Tanzania:

  1. Benki ya Dunia
  2. Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na UKIMWI Kifua Kikuu na Malaria
  3. Shirika la Misaada la Ubelgiji
  4. Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kudhibiti UKIMWI
  5. Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa
  6. Mpango wa Chakula Duniani
  7. Shirika la Afya Duniani
  8. Shirika la Kilimo la Umoja wa Mataifa
  9. Ubalozi wa Ufaransa
  10. Idara ya Maendeleo ya Uingereza
  11. Shirika la Maendeleo la Uswidi
  12. Shirika la Misaada la Japan
  13. Shirika la Maendeleo la Canada
  14. Shirika la Maendeleo la Norway
  15. Shirika la Maendeleo la Ireland
  16. Shirika la Maendeleo la Denmark
  17. Ubalozi wa Falme ya Uholanzi
  18. Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa
  19. Mfuko wa Idadi ya Watu wa Umoja wa Mataifa
  20. Seikali ya Marekani
  21. Umoja wa Nchi za Ulaya
  22. Shirika la Misaada la Ujerumani
  23. Shirika la Maendeleo la Uswisi

 

 
Asasi za Kiraia (AZAKI) Print

Sekretarieti za Mikoa (RSs) zimepewa jukumu la uratibu, usimamizi na kurahisisha kazi kwenye wilaya na jamii.

Kuundwa kwa Wakala za Uwezeshaji za Mikoa. (RFAs), kila moja ikiwakilisha mikoa miwili ilikuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha msaada wa kiufundi na kifedha unaotolewa wilayani na kwenye jamii. RFAs zinaonekana kama macho, masikio na mikono ya TACAIDS. Ziliweza kuchochea kwa kiasi kikubwa, mwitikio wa wilayani kupitia kujenga uwezo na kuelekeza fedha kwenye CSOs. Pia zimekuwa zikitoa msaada wa kiufundi kwa RSs na CMACs. Hata hivyo RFAs zimekuwa changamoto kubwa katika kufikia na kutoa huduma katika mikoa miwili inayoshughulika nayo. Hili lilikuwa tatizo lililosababisha changamoto kwa upande wa ununuzi na usafirishaji, kudhibiti muda na utoshelevu wa rasilimali. Zaidi ya hayo, kutokana na kwamba RFAs hazikuwa kwenye muundo wa serikali, ilisababisha wakati mwingine kutiliwa shaka na wadau katika ngazi ya mikoa na hivyo kuonekana kama chombo mbadala au pinzani.

Read more...
 
TAF Print

Mtandao wa Asasi Zinazoshughulikia UKIMWI Tanzania

 
Asasi za Kidini Print

Sekretarieti za Mikoa (RSs) zimepewa jukumu la uratibu, usimamizi na kurahisisha kazi kwenye wilaya na jamii.

Kuundwa kwa Wakala za Uwezeshaji za Mikoa. (RFAs), kila moja ikiwakilisha mikoa miwili ilikuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha msaada wa kiufundi na kifedha unaotolewa wilayani na kwenye jamii. RFAs zinaonekana kama macho, masikio na mikono ya TACAIDS. Ziliweza kuchochea kwa kiasi kikubwa, mwitikio wa wilayani kupitia kujenga uwezo na kuelekeza fedha kwenye CSOs. Pia zimekuwa zikitoa msaada wa kiufundi kwa RSs na CMACs. Hata hivyo RFAs zimekuwa changamoto kubwa katika kufikia na kutoa huduma katika mikoa miwili inayoshughulika nayo. Hili lilikuwa tatizo lililosababisha changamoto kwa upande wa ununuzi na usafirishaji, kudhibiti muda na utoshelevu wa rasilimali. Zaidi ya hayo, kutokana na kwamba RFAs hazikuwa kwenye muundo wa serikali, ilisababisha wakati mwingine kutiliwa shaka na wadau katika ngazi ya mikoa na hivyo kuonekana kama chombo mbadala au pinzani.

Kuanzishwa kwa shughuli za UKIMWI wilayani, vijijini, na kata kunahitaji rasilimali endelevu kwa upande wa mafunzo, usimamizi na msaada wa kiufundi. Matumizi ya Kanuni ya Dhana Tatu katika ngazi ya wilaya yameonyesha kuwa changamoto kubwa kwa watendaji wote kutokana na kukosa uzoefu katika mipango shirikishi na uunganishaji pamoja na kuchangia majukumu baina ya sekta mbalimbali. Ushirikishaji wa CSo, katika mipango ya halmashauri unahitaji kuimarishwa, wakati kuaminiana na kusaidiana miongoni mwa watendaji mbalimbali kunahitaji kuendelezwa.

Katika ngazi ya jamii, kuna maelfu kadha ya mashirika ya kijamii (CBOs), pamoja na Mashirika ya Dini (FBos). Hivi vimetoa mchango mkubwa katika Mwitikio wa Taifa, hasa mahali ambapo kulikuwa na fedha na msaada wa kiufundi kupitia asasi zisizo za serikali (AZISE). Nyingi za asasi hizi pia zinajihusisha na ART. Pamoja na idadi yao, uwezo na ubora wa huduma na afua zinazotolewa na CBOs hizo vinatofautiana sana. Uzingatiaji wa miongozo mizuri na ushirikishaji katika jamii pamoja na mipango ya wilaya ni changamoto zinazohitaji kufanyiwa kazi.

 
More Articles...
<< Start < Prev 1 2 Next > End >>

Page 1 of 2