The Tanzania Commission for AIDS
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Ofisi ya Waziri Mkuu

TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA
The Tanzania Commission for AIDS
TACAIDS
| English | 
Kamati ya Taifa ya Ushauri wa Utafiti Print

Kamati ya Taifa ya Ushauri wa Utafiti ina wajumbe kutoka kwenye Wizara, Asasi za Utafiti, Asasi za Elimu ya Juu na Asasi zisizo za kiserikali za Kitaifa na Asasi za Jinsia.


Wajumbe wa  Kamati hiyo wanatoka:

  1. Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OWM-TAMISEMI)
  2. Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS)
  3. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
  4. Wizara ya Sheria na Katiba
  5. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
  6. Chuo Kikuu cha Tiba na Sayansi za Jamii, Muhimbili (MUHAS)
  7. Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA)
  8. Chuo cha Maendeleo ya Jamii, Tengeru, Arusha
  9. Mtandao wa Jinsia Tanzania  (TGNP)
  10. Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC)
  11. Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya Tanzania
  12. Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TDFA)
  13. Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF)
  14. Taasisi ya Utafiti kuhusu Kupunguza Umaskini (REPOA)


Wajumbe wengine wanaweza kualikwa kadri itakavyoonekana inafaa.

 

Majukumu ya Kamati ya Taifa ya Ushauri wa Utafiti

  1. Kubainisha utafiti wa maeneo makuu ya VVU/UKIMWI yanayoweza kufanyiwa kazi kila la mwaka
  2. Kuanzisha mipango mahsusi ya kuharakisha ugharimiaji wa utafiti kuhusu VVU/UKIMWI
  3. Kuhakikisha kuwa upatikanaji wa fedha unafahamika kwa watafiti na kutengwa kwa mujibu wa Ajenda ya Taifa ya Utafiti wa VVU/UKIMWI
  4. Kutoa na kuongoza mfumo wa utafiti wa kitaifa kwa ajili ya utekelezaji, ufuatiliaji na ushirikiano wa shughuli za utafiti wa VVU/UKIMWI
  5. Kutayarisha utaratibu unaoeleweka wa namna ya kuratibu, kufuatilia na kuanzisha uhusiano na asasi za utafiti na kuwa na uelewa wa pamoja
  6. Kusaidia kama za ruzuku za TACAIDS kuhusu aina gani ya utafiti upewe fedha, pia kuweza kujua orodha ya utafiti uliokwishafanywa ili kupunguza kujirudia kwa shughuli miongoni mwa wadau wa utafiti
  7. Kusaidia TACAIDS katika kupitia mapendekezo ya utafiti yaliyopelekwa kwa vyombo vinavyohusika na kuharakisha kuidhinishwa ili kupunguza muda mrefu wa kusubiri kukutana kwa Bodi inayohusika
  8. Kuhimiza na kuimarisha uhusiano vyombo vingine vya utafiti
  9. Kuanzisha orodha na hali ya tafiti zilizofanywa kuhusu VVU/UKIMWI nchini Tanzania kwa manufaa ya watunga sera
  10. Kuanzisha na kuendeleza utaratibu wa uenezaji unaofaa wa matokeo ya utafiti kisanyansi na kwa lugha rahisi inayoelewaka ili kuepuka utata katika kueleweka kwa matokeo ya utafiti kwa Watanzania wa kawaida wanaohitaji kutumia matokeo hayo kwa kuboresha afya na ustawi.