Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi akiambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania- Tacaids, Dkt. Adam Mrisho, pamoja na wadau wengine, ametembelea ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kufuatilia taarifa kuhusu utekelezaji wa shughuli za VVU na UKIMWI. Ambapo ameuelezea Mkoa huo kuwa umeendelea kupiga hatua katika kupunguza maambukizi mapya na kuimarisha mwitikio dhidi ya VVU na UKIMWI