Katika maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania-TACAIDS, Dr. Adam J Mrisho, ametembelea banda la TACAIDS na kujionea huduma mbalimbali zinazoendelea kutolewa kwa jamii, ikiwemo elimu ya kinga dhidi ya VVU pamoja na huduma za upimaji.